Thursday, May 2, 2013

Wosia wa jay dee kama akifa kabla ya Ruge au Joe Kusaga

Lady jay dee
Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi
Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa.

Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari.

Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki.

Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa.
Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao.

Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria.
Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu.

Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia.
Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa.

Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao.
Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni.

Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu.

Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame
Enyi mtakaokuwa hai baada yangu.

Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai
Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu.
Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia.

Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge.
Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka.

Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia..
Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star..

Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??.
Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu.

Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili.
Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri.
Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani??
Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi??

Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili.

Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu.
Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma??
Roho gani hiyo??

Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu.Soure Jamii forum

Wednesday, May 1, 2013

Ajali mbaya yatokea Chalinze

Taarifa mpaka sasa zilizotufikia ajali mbaya imetokea mjim wa pwani Chalinze na Mpaka sasa hakuna taarifa kwa kuwepo yoyoyte aliyepoteza Maisha ila wapo waliojeruhiwa lakini mpaka sasa wana uzalendo wanafatilia ili kupata Taarifa zaidi kujua hali ya Majeruhi na kuona Wanaendeleaje

SENETA MUTULA KILONZO WA KENYA AFARIKI DUNIA

Seneta Mutula kilonzo
Kwa mujibu wa mmoja wa wanafamilia ambae ameongea na Capital FM Nairobi, Mutula amekutwa akiwa amefariki dunia nyumbani kwake Machakos, hakuwa anaugua…
Marehemu Mutula kilonzo                                 

Chadema yamtuhumu Kinana kuhusika na biashara ya pembe za ndovu

Abdulrahman Kinana 
Dodoma. Kambi ya Upinzani Bungeni imetoa tuhuma nzito kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ikidai kuwa anajihusisha na mtandao wa ujangili nchini.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi amejibu tuhuma hiyo akisema ni za uongo huku akiituhumu kambi hiyo kuwa imedanganya wakati inajua ukweli kuhusu tuhuma dhidi ya Kinana.
Akiwasilisha maoni ya upinzani kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2013/14, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Maliasili, Mchungaji Peter Msigwa alisema vitendo vya ujangili vimekuwa vikilitia doa taifa kwenye jumuiya za kimataifa.
“Kwa bahati mbaya ni kwamba wahusika wengi ambao wanatajwa kwa ushahidi ni makada maarufu na wengine ni viongozi waandamizi wa CCM,” alisema Mchungaji Msigwa.
“Tumeshuhudia watuhumiwa wengine wa ujangili ambao Ikulu imediriki kuwapatia nafasi kubwa za uongozi wa taifa hili, licha ya kutajwa kwenye ripoti ya uchunguzi kuhusiana na ujangili.”
Alisema mwaka 2009, meli ya Kampuni ya Wakala wa Meli ya Sharaf Shipping inayomilikiwa na Kinana ilikamatwa China ikiwa na makontena yenye nyara za Serikali ikiyasafirisha kwenda Hong Kong.
“Nyaraka zilizopo Ofisi za Wakala wa Usajili wa Kampuni na Biashara (Brela), zinaonyesha kuwa kampuni hiyo ya Kinana ilisajiliwa Oktoba 2003 na kupewa hati na. 47221.
“Nyaraka zinaonyesha kuwa Kinana anamiliki hisa 7,500 kati ya 10,000 za kampuni hiyo iliyosajiliwa Dar es Salaam. Mshirika mwenzake katika kampuni hiyo, Rahma Hussein ambaye ni mke wake anamiliki hisa 2,500,” alisema Msigwa.

Dk Nchimbi ajibu mapigo
Akijibu tuhuma hizo, Waziri Nchimbi alisema: “Ukiona mtu anasimama na kuamua kusema kuwa hakuna kinachofanywa na wizara kuhusu masuala ya ujangili, ni wazi uelewa wake unakuwa na utata mkubwa.”
Alisema hoja zilizojengwa dhidi ya Kinana ni uongo mtupu... “Nimejaribu kufuatilia kwa makini alichokisema alikimaanisha, alikielewa, alikitafakari au aliandikiwa tu akaenda kusoma? Baada ya kutafakari kwa kina nikagundua hakuwa na nia mbaya, aliandikiwa tu na ameenda kusoma,” alisema Dk Nchimbi.
Alisema ukweli wa jambo hilo ni kwamba ipo tofauti ya majukumu ya kampuni za Wakala wa Meli na shughuli za kupakia mizigo bandarini huku akituhumu kambi ya upinzani kuwa inajua ukweli lakini imeamua kupotosha umma.
Dk Nchimbi ambaye alikuwa mchangiaji wa kwanza, alisema wakala hawezi kuwa mmiliki wa meli, bali anamwakilisha mwenye meli kwenye shughuli ndogondogo zinazofanyika inapofika nchi fulani kama kuhudumia watumishi wa meli, mahitaji muhimu na kufanya usafi.
“Lakini kuna watu wanaitwa ‘clearing and forwarding (Kupakua na kupeleka mizigo). Napenda kukwambia Mchungaji Msigwa kuwa kazi yao ni kupeleka na kutoa mizigo bandarini,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza;
“Kule ndiko kuna utaratibu wa upekuzi, katika utaratibu wa upekuzi mtu wa ‘shipping agency’ (wakala wa meli) hahusiki, sina shaka hata kidogo Mchungaji Msigwa analijua hili ninalolisema, ila amelifumbia macho kwa makusudi kwa masilahi yasiyokubalika katika taifa.”
Alisema kumekuwa na uvumi ambao umekuwa ukifanywa kwa makusudi kuwa Kinana anahusika na meli iliyohusika kusafirisha pembe zile.
“Uvumi huu ni uzushi, meli iliyobeba mizigo ile inaitwa Delmas Nakadha, mmiliki wake anaitwa Bus Herman Ledley jambo hili Kambi ya Upinzani Bungeni inalijua, ila kwa masilahi yasiyokubalika katika taifa wameamua kupotosha Bunge lako,” alisema.
Alisema baada ya uchunguzi wa kutosha, wahusika walibainika na ikafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi namba 3 na 4 ya mwaka 2009 kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.
“Hawa (anawataja) ndiyo waliopelekwa kortini, uchunguzi ulijidhihirisha kuwa ndiyo watuhumiwa wa jambo hili, Kambi ya Upinzani Bungeni inalijua,” alisema:SOURCE MWANANCHI
Abdulrahman Kinana

Tuesday, April 30, 2013

KAZI KWAKO


Je Madrid watafanikiwa kupita leo wakiwa nyumbani?

 Koccha wa Real Madrid Jose Mourinho

Team ya Madrid leo watashuka dimbani huku wakiwa na deni la magoli matatu bila ili kujiwezesha kuvuka na kutinga fainali..ila wakilishi hao wa spain watakuwa na kazi ngumu ya kutafuta namna ya kuwabana MARIO GOTZE na ILKAY GUNDOGAN.

Mbali na madrid kuanzisha miamba yake leo kipind cha mwanzo CR7,ANGEL DIMARIA akifuatiwa  GONZALO HIGUAN bdo real madrid watakuwa na kazi ngumu ya kushinda na kufanikiwa wapinzani wao wasiweze kufunga ambalo ni jambo gumu kama kuwazuia kina REUS na ROBERT LEWANDOWSKI.

Jambo ambalo Mourinho leo atakuwa analipa kipaumbile zaidi ni mashambulizi ili kuhakikisha wanapata ushindi wa zaidi ya magoli matatu tena bila kufungwa na kwa mabeki wa real madrid ni jambo gumu na wala si jepesi kuwazuia Dortimund kuondoka bila kupata goli moja ili hali kila jambo linawezekana katika mpira
Mshamuliaji wa Borrusia Dortimund R.Lewandowski
Mashabiki wengi leo wa real madrid watakuwa wanamuhofia huyu jamaa japokuwa watakuwa wanamkaribisha santiago Bernabeu mechi iliyopita alifunga magoli manne peke yake moja likipatikana kwa njia ya penatu
real madrid wakiwa mazoezini kujiandaa na mechi
Real Madrid Borussia Dortmund
Won, 3-2 vs. Manchester City (H) Won, 1-0 vs. Ajax (H)
Won, 4-1 vs. Ajax (A) Draw, 1-1 vs. Manchester City (A)
Loss, 2-1 vs. Borussia Dortmund (A) Won, 2-1 vs. Real Madrid (H)
Draw, 2-2 vs. Borussia Dortmund (H) Draw, 2-2 vs. Real Madrid (A)
Draw, 1-1 vs. Manchester City (A) Won, 4-1 vs. Ajax (A)
Won, 4-1 vs. Ajax (H) Won, 1-0 vs. Manchester City (H)
Draw, 1-1 vs. Manchester United (H) Draw, 2-2 vs. Shakhtar Donetsk (A)
Won, 2-1 vs. Manchester United (A) Won, 3-0 vs. Shakhtar Donetsk (H)
Won, 3-0 vs. Galatasaray (H) Draw, 0-0 vs. Malaga (A)
Loss, 3-2 vs. Galatasaray (A) Won, 3-2 vs. Malaga (H)
Loss, 4-1 vs. Borussia Dortmund (A) Won, 4-1 vs. Real Madrid (H)
kama madrid leo watashinda itakuwa furaha sana katika jiji la madrid na furaha kubwa kwa C.Ronaldo ukiangalia dunia nzima itakuwa inatima leo atafanya nini kuisaidia team yake na kuinusuru kutoka kwenye michuano hiyo
C.Ronalo   
 

Monday, April 29, 2013

Diamond na kauli ya kukera kwa mashabiki

MSAFI DIAMOND AKIWA NA WACHEZA SHOW WAKE LONDON


     Habari wanauzalendo wenzang kwanza poleni na majukumu ya hapa na pale na hongereni kwa kushiriki pamoja katika harakati za kujikomboa na hali ngumu katika maisha.
    Nisengependa kuwachosha na maneno binafsi nimesikitishwa na ujumbe mfupi uliotolewa na msanii maarufu hapa nchini anayeshika nyoyo za wananchi hasa kina dada,Mamiss,Warembo,vijana na Wazee kwa ujumla sio siri msafi huyu anajua ila kwa kauli ya leo niliyoisoma kwenye ukurusa wake wa facebook imenisikitisha sana na nukuu:NASHANGAZWA KWA MITAIRA MENGINE YAN KWA KUPONDA NAMBA MOJA 1 ILA KWA PLATINUM WATASURRENDER AF LONDON NIMEFIKA KWA BIDII YANGU SO HATA MKIPONDA KAZI BURE MUNGU PEKEE NDO ANA UWEZO WA KILA JAMBO SO WEWE TUMBILI.

Hakika hii si kauli hasa kwa Diamond kwenda kwa mashabiki wake ukizingatia wao ndio waliomfkisha hapo alipo na kufanya yeye aseme hivyo leo kwa kweli ina kera sana na si jambo la kuchekewa kabisa.Mimi naamin Diamond ni msanii mzuri na ni kweli ana bidii ila kazi yake hiyo afanye mpaka atoke machozi ya damu bila mashabiki hakuna Diamond nja wala hakuna wasafi kitendo hiki alichofanya  binafsi siungi mkono na wala si mpongezi tena inabidi aumbe radhi mashabiki wake.

Diamond akiwa katika mahojiano na kipindi cha SPORAH TALK SHOW







   USHAUR;Diamond ni msanii mzuri na anayezingatia kazi zake kwa kuzingatia hilo sisi mashabiki wake tunaomba scandal zisisaidie kubeba uwezo wake kuna mambo anatakiwa ayasamehe ikiwezekana ayaachane nayo kabisa ukizingatia yeye ni kioo cha jamii na mfano wa kuigwa na baadhi ya vjana

Saturday, April 27, 2013

UJUMBE MFUPI AMBAO MH. JOSHUA NASSARI AMEMTUMIA MKUU WA MKOA WA ARUSHA LEO KUHUSIANA NA MATUMIZI YAKE MABAYA YA MADARAKA KUMGANDAMIZA MH LEMA

Mhe. RC Salaam. Ninasikishwa sana na mambo yanayoendelea mkoani kwangu Arusha. Lakini pia nasikitika kwamba na wewe umeamua kuwa sehemu ya uonevu dhidi ya utu na haki. Hatuwezi kuvumilia movement yeyote, ya awaye yeyote yule dhidi ya kweli na usawa. " We will stand for justice, anytime, anywhere at any cost. Video zinaonyesha jinsi ambavyo lema alisaidia kutuliza jazba za wanafunzi wa uhasibu, jinsi alivyowaasa bila woga kuhusu life style yao na umuhimu wa discpline katika maisha! Kama kiongozi mwenye dhamana ya ulinzi na usalama wa mkoa ulipaswa ku-appreciate. Kinachoendelea ni yale niliyowahi kukushauri kama sio kukuonya juu ya juhudi kubwa za viongozi wa ccm na ofisi yako kutu-undermine wabunge wa chadema arusha hususani mimi na mhe. lema na ukaahidi kubadilika. Tuliaminiwa na maelfu ya watu wakatuchagua, hatupo tayari kusaliti imani hii. Najua kuna hofu kubwa kwa sababu ya chaguzi zijazo za madiwani arusha. Nipo dodoma lakini nalazimika kuja ofisini kwako jumatatu, kukushauri tena kwa mara nyingine. Kama mnaweza kumfanyia hivi mbunge, itakuwaje kwa machinga wa ngarenaro au mama ntilie wa usa river?? Nikutakie siku njema. Joshua Nassari (MB) April 27, 2013. Dodoma Joshua Nassari, Member of Parliament and Shadow Minister for Communication, Science&Technology Tanzania.

Shilole abanwa kuhusu kutongoza vjana wadogo

Wiki iliyopita katika safu hii tulimtambulisha kwenu msanii wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, kama kawaida maswali mengi yaliulizwa kama ifuatavyo: KWELI ALIOLEWA?
Eti ni kweli uliolewa na ulikuwa unaishi Keko? Khatibu, Dar, 0715456296.
SHILOLE: Kweli.
TABIA YA KUTONGOZA SERENGETI BOYS
Shilole acha kutongoza watoto wadogo halafu sauti ya kuimba huna, acha fani za watu. Sister Havinitishi, Dar, 0655196161.
SHILOLE: Mimi kwanza ni mdogo na siwatongozi watoto wadogo, kuhusu kuimba nitajifunza zaidi.
KUHUSU BABA WATOTO WAKE
Dada Shilole uko juu nakupa big up! Ningependa kufahamu hao watoto wako umezaa na baba mmoja au kila mtoto ana baba yake? Angel, Dar, 0714600415.
SHILOLE: Asante, watoto wangu kila mmoja ana baba yake.
HUYU AMEMZIMIA
Shilole naomba namba ya simu maana unanikosha wewe ni mzuri sana. Sangoti, Korogwe, 0654848387
SHILOLE: Asante, nitakutafuta.
KUHUSU MIDUME MCHARUKO MTAANI
Shilole wewe ni msanii mahiri kunako kiwanda cha filamu na muziki Bongo, je, unajiepusha vipi na midume inayokutokea kimapenzi? Salim Liundi, Dar, 0658110395.
SHILOLE: Asante, huwa najiepusha na midume kwa kujiheshimu na kujilinda hivyo siwapi nafasi.
UHUSIANO WAKE NA NGASSA
Shilole nataka kujua eti wewe na kiungo mahiri wa timu ya Simba Mrisho Ngassa mnatoka kimapenzi, mbona kuna tetesi za ajabu kitaani? Msomaji.
SHILOLE: Siyo kweli.
MZAZI MWENZAKE VIPI?
Umesema una watoto wawili, je vipi kuhusu mzazi mwenzio uko naye au ndiyo umemtema baada ya kupata umaarufu? Shariff Juma, Dar, 0713332349.
SHILOLE: Siko naye.
BIFU LAKE NA FLORA
Shilole hongera kwa kazi zako unajitahidi ila nataka kujua kwa nini hupatani na Flora Mvungi.  Silla, Dar, 0718764242.
SHILOLE: Asante, mimi sijagombana na mtu ila mti wenye matunda siku zote lazima upigwe mawe.
KUFICHA WATOTO WAKE
Zamani ulikuwa unaficha kama una watoto wawili mpaka mtu wako wa karibu alipotoa hiyo siri, kwa nini ulifanya hivyo? Cassian, 0655202202.
SHILOLE: Siyo kweli mbona watoto wangu wapo wazi!
KUHUSU MKOROGO
Big up! Shilole napenda muziki wako ushauri wangu kwako acha mkorogo unakuharibu. Tina, Mwanza, 0719747965.
SHILOLE: Siku hizi sipaki mkorogo, nimeacha.
SKENDO YA KUTOKA NA RAY
Dada Shilole unafanya kazi nzuri ila punguza skendo nasikia ulishawahi kutembea na Ray, je ni kweli? Charles Mallya, Mwanza, 0759022399.
SHILOLE: Asante, sijawahi kutembea na Ray.
BARNABA JE?
Shilole hivi ni kweli ulikuwa unatembea na Barnaba na kwa sasa mpenzi wako ni nani? Musa Mbughi, Sumbawanga, 0764021259.
SHILOLE: Siwezi kusema chochote.
UKWELI KUHUSU KUBAKWA
Shilole najua mtoto wako wa kwanza umezaa na Makala wa Igunga Tabora na ulikuwa unaishi naye kwa Tatu Balozi, ilikuwaje ukasema mwanaume aliyekupa mimba ya kwanza alikubaka? Ibrahim Yusuph, Dar, 0719599195.
SHILOLE: Sipendi kurudi nyuma ila ni kweli alinibaka nikapata ujauzito.
HISTORIA YAKE KWA UFUPI
Dada nataka kujua historia yako kiufupi. Sultan, Dar, 0654324222.
SHILOLE: Nimezaliwa Igunga Tabora nikiwa mtoto wa mwisho, sanaa nilianza mwaka 2010.

JTF kill top Boko Haram commander, Mohammed Chad

The JTF Spokesman Leuitenant Colonel Sagir Musa in Maiduguri last night said, a special operation was conducted at Ruwan – Zafi area of Maiduguri metropolis by troops of the JTF Operation RESTORE ORDER and operatives of the department of State Security Service (SSS) at about 3:00 am on Friday 26 April, 2013 “led to the death of a notorious Boko Haram terrorist a.k.a Mohammed Chad, an indigene of Marte, Borno State that has been on the wanted list of the JTF”.
He added that intelligence indicated that he was involved in the planning/execution of many terror attacks in and outside Borno State. For instance, he masterminded the attack on Sanda Kyarimi Secondary Schools located at Ruwan Zafi, where they killed a teacher and injured 3 female students on 18 March 13.
Sagir however stated that the suspect is believed to be the successor to Ba,ana Assalafi a key Boko Haram Commander that lost his life during a shoot out with security agencies in Sokoto on 13 March 2013.

 Mohammed Chad, a top Boko Haram Commander and an indigene of Marte Local Government Area of Borno State who has been on the wanted list of the Joint Task Force (JTF) has been killed in a shootout with JTF and men of the SSS at Ruwan Zafi of Maiduguri Metropolis in Borno.

MAKOSA YALIYOMFANYA LEMA KUNYIMWA DHAMANA

Mambo yaliyomfanya Mbunge wa arusha Godbless Lema akamatwe na kunyimwa dhamana jioni hii ni haya yafuatayo baada ya kuongea na Mwanasheria wa Lema wakili Humphrey Mtui

i)Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘.Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa(Worth fighting for)

ii)Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off.Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’Kwa hiyo huo ni uchochezi

iii)Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’Huu nao umeitwa kwamba ni uchochezi.

Sasa haya maneno hapo juu ndiyo yaliyosababisha jeshi la polisi kuvamia nyumbani kwake usiku wa manane na kuzua taharuki maeneo hayo na ndani ya nyumba yenye ndugu jamaa na hata mtoto mwenye miezi mitano huku polisi wakitumia nguvu na kukiuka sheria

Huo umeitwa uchochezi baada ya mkuu wa mkoa kumtumia ujumbe wa mkononi kupitia simu yake kupitia namba 0752960276 aliyotishia kumbambikizia kesi anayoitaka yeye.

Sasa hayo waliyoita makosa ya uchochezi ndiyo yaliyomnyima haki ya dhamana leo.tutafakari kama Arusha itatawalika kwa hali hii.

Hebu tupime makosa hayo matatu kama yanaweza ku-justfy mambo yote yaliyotokea
.