UJUMBE MFUPI AMBAO MH. JOSHUA NASSARI AMEMTUMIA MKUU WA MKOA WA ARUSHA LEO KUHUSIANA NA MATUMIZI YAKE MABAYA YA MADARAKA KUMGANDAMIZA MH LEMA
Mhe.
RC Salaam. Ninasikishwa sana na mambo yanayoendelea mkoani kwangu
Arusha. Lakini pia nasikitika kwamba na wewe umeamua kuwa sehemu ya
uonevu dhidi ya utu na haki. Hatuwezi kuvumilia movement yeyote, ya
awaye yeyote yule dhidi ya kweli na usawa. " We will stand for justice,
anytime, anywhere at any cost. Video zinaonyesha jinsi ambavyo lema
alisaidia kutuliza jazba za wanafunzi wa uhasibu, jinsi alivyowaasa bila
woga kuhusu life style yao na umuhimu wa discpline katika maisha! Kama
kiongozi mwenye dhamana ya ulinzi na usalama wa mkoa ulipaswa
ku-appreciate. Kinachoendelea ni yale niliyowahi kukushauri kama sio
kukuonya juu ya juhudi kubwa za viongozi wa ccm na ofisi yako
kutu-undermine wabunge wa chadema arusha hususani mimi na mhe. lema na
ukaahidi kubadilika. Tuliaminiwa na maelfu ya watu wakatuchagua, hatupo
tayari kusaliti imani hii. Najua kuna hofu kubwa kwa sababu ya chaguzi
zijazo za madiwani arusha. Nipo dodoma lakini nalazimika kuja ofisini
kwako jumatatu, kukushauri tena kwa mara nyingine. Kama mnaweza
kumfanyia hivi mbunge, itakuwaje kwa machinga wa ngarenaro au mama
ntilie wa usa river?? Nikutakie siku njema. Joshua Nassari (MB) April
27, 2013. Dodoma Joshua Nassari, Member of Parliament and Shadow
Minister for Communication, Science&Technology Tanzania.
No comments:
Post a Comment